Tetesi za Soka Ulaya Jumamosi 31.08.2019:

 Zaha, Darmian, Pogba, Sancho, Neymar, Eriksen, Ozil

Wilfried ZahaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMshambuliaji wa Ivory Coast forward,Wilfried Zaha
Mwenyekiti wa Crystal Palace Steve Parish amesema atamruhusu mshambuliaji wa Ivory Coast forward Wilfried Zaha, 26, kuondoka klabu hiyo msimu ujao wa uhamisho wa wachezaji- ikiwa dau lililotangazwa na Arsenal na Everton litafikiwa. (Daily Mail)
Parma wamekubali mpango wa kumsajili beki wa Manchester United Matteo Darmian kw euro milioni 1.4 (Sky Sports)
Kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane amekasirishwa na hatua ya viongozi wakuu wa klabu hiyo kushindwa kumsajili Paul Pogba,26, kutoka Manchester United. (Sports)
Neymar ameifahamisha Paris St- Germain kuwa yuko tayari kurudi chini na kuboresha uhusiano wao endapo atakosa nafasi ya kuhamia Barcelona ama Real Madrid kabla dirisha la uhamisho wa wachezaji Ulaya kufungwa msimu huu.( Independent)
NeymarHaki miliki ya pichaAFP
Image captionNeymar, nyota wa soka wa kimataifa wa Brazil
Huku hayo yakijiri, mkurugenzi wa kiufundi wa Paris St-Germain Leonardo amesema mabingwa hao wa Ufaransa hawajakaribia kufikia makubaliano na Barcelona kumhusu Neymar. (Marca)
Meneja wa klabu ya Barcelona Ernesto Valverde amesema kuwa amechoshwa na mashauriano yanayozunguka uhamisho wa Neymar kuja klabu hiyo (Standard)
Mkufunzi wa Arsenal Unai Emery amesema kuwa mlango upo wazi kwa kiungo wa kati wa klabu hiyo Mesut Ozil kurejesha hadhi ya mchezaji nyota wa Gunners.(Mirror)
Mesut Ozil
Image captionMesut Ozil, Kiungo wa kati wa Arsenal
Paris St-Germain wamewatambua wachezaji kiungo wa kati wa Tottenham Christian Ericksen 27, na mshambuliaji wa Juventus Paulo Dybala,35,kama wachezaji wawil8 watakao chukua nasi ya Neyma endapo atahamia Barcelona (Le Parisien kwa kifaransa)
Atletic Madrid wanatafakari uwezekano wa kusajili kwa mkopo mshambuliaji wa Inter Milan Mauro Icadi na baadae kumnunua kwa euro milioni 70 (ESPN)
Real Madrid imekubali kuiuzia Paris St-Germain kipa wake Keylon Navas,32, ikiwa klabu hiyo itakubali kumuachilia Alphonse Riola kujiunga nao kwa mkopo (Star)
Mauro IcadiHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMshambuliaji wa Inter Milan Mauro Icadi
Mshambuliaji wa zamani wa Tottenham Fernando Llorente,34, amekubalia kutia saini mkataba wa miaka miwili na Napoli inayoshiriki Ligi Kuu ya Italia, Serie A (Sky Sports)
Kiungo wa Kati wa Sportings Bruno Fernandes aliyehusishwa na tetesi za uhamisho kwenda Manchester United na Tottenham msimu wa joto hatimae ametua Real Madrid baada ya kutiavsaini mkataba wa euro milioni 63 (Mail)

Tetesi Bora Ijumaa

Paris St-Germain inamtaka kiungo wa kati wa Tottenham Christian Eriksen mwenye umri wa miaka 27, kama mchezaji atakayeichukua nafasi ya mchezaji wa timu ya taifa ya Brazil Neymar, anayekaribia kurudi Barcelona. (Le Parisien)
Paul PogbaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionPaul Pogba
Mchezaji wa kiungo cha kati wa Manchester United na timu ya taifa ya Ufaransa Paul Pogba, mwenye umri wa miaka 26, hatosaini kuongeza mkataba wake hivi sasa na anataka kujiunga na Real Madrid haraka iwezekanavyo. (Marca)
Bosi wa Tottenham Mauricio Pochettino anasua sua kumuita mlinzi wa timu ya taifa ya Ivory Coast Serge Aurier kwa Derby ya London kaskazini siku ya Jumapili huko Arsenal wakati mchezaji huyo wa miaka 26 akiwa anaweza kuondoka kabla ya kufungwa dirisha la uhamisho Ulaya Jumatatu. (Evening Standard)
Mauricio PochettinoHaki miliki ya pichaREX FEATURES
Mlinzi wa Barcelona Gerard Pique anatumai kuwa Harry Maguire ataweza kuisaidia klabu yake ya zamani Manchester United kushinda taji la ligi kuu ya England. (Express)
Aliyekuwa mshambuliaji wa Manchester United Romelu Lukaku, mwenye umri wa miaka 26, amepunguza uzito wa mwili baada ya kufuata muongozo wa lishe chini ya meneja Antonio Conte tangu raia huyo wa Ubelgiji kujiunga na Inter Milan. (Mail)
Arsenal dhidi ya Tottenham inajitayarisha kuipiku Liverpool dhidi ya Everton katika mchezo mkali wa Derby katika ligi kuu ya England. (Sun)

Post a Comment

0 Comments