Rais Magufuli amjulia hali Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dar


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Madaktari wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili pamoja na Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) wakimuombea Sala Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dar es Salaam Mhashamu Yuda Thadeus Ruwa’ichi ambaye anapatiwa matibabu katika Taasisi hiyo ya MOI mara baada ya kufanyiwa upasuaji wa Kichwa
Rais wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemjulia hali Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dar es Salaam Mhashamu Yuda Thadeus Ruwa’ichi anayepatiwa Matibabu katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI).

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Madaktari wa Muhimbili pamoja na MOI mara baada ya kumjulia hali Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dar es Salaam Mhashamu Yuda Thadeus Ruwa’ichi ambaye amelazwa katika Taasisi hiyo ya MOI

Post a Comment

0 Comments