Atal, Sane, Fekir, Mkhitaryan, Wenger
Manchester City inajaribu kumshawishi mshambuliaji wake Leroy Sane, 23, kutia saini kandarasi mpya kabla ya Bayern kupewa fursa nyengine ya kuwasilisha ombi la kumsaini raia huyo wa Ujerumani . (Standard)
Chelsea itajaribu kumsaini beki anayedaiwa kuwa na thamani ya £35m kutoka klabu ya Nice Youcef Atal, raia wa Algeria mwenye umri wa miaka 23 mwezi Januari iwapo watafanikiwa kuondolewa marufuku yao ya uhamisho kuanzia mwanzo wa 2020. (Sun)
Manchester United inamnyatia kiungo wa kati wa Benfica na Portugal Florentino Luis, 21, lakini anaweza kukabiliwa na ushindani wa kumsaini kutoka kwa klabu ya Manchester City (A Bola via Sport Witness - in Portuguese)
Kiungo wa Real Betis na Ufaransa Nabil Fekir, 26, amekana madai kwamba uhamisho wake wa dau la £53m kuelekea Liverpool 2018 uligonga mwamba kutokana na kufeli kwa vipimo vya matibabu.. (L'Equipe, via Talk Sport)
Manchester City ilifeli katika ombi lake la kumsaini beki wa inter Milan raia wa Slovakia Milan Skriniar, 24, lakini inaweza kujaribu tena mwezi Januari. (Tuttosport, via Sport Witness)
Kiungo wa kati wa Armenia ambaye aliwahi kuzichezea Manchester United na Arsenal Henrikh Mkhitaryan, 30, ambaye kwa sasa anaichezea klabu ya Roma amesema kwamba kipindi chake cha mchezo katika ligi ya Premia kilimfanya kukosa mapenzi na kandanda. (Manchester Evening News)
Chelsea itajaribu kumsaini beki wa kushoto wa Valencia na Uhispania Jose Gaya, 24, wakati marufuku ya dirisha la uhamisho itakapokamilika msimu ujao. (Soccer Link, via Talk Sport)
Beki wa zamani wa Arsenal na Ujerumani Per Mertesacker, 34, anaamini wachezaji wa klabu hiyo walishindwa kutoa ushahidi wa kuwepo kwa imani ya Wenger katika siku za mwisho za mkufunzi huyo wa zamani wa Arsena(Standard)
Kiungo wa kati wa Brazil Lucas Piazon, 25, anasema yuko tayari kuondoka Chelsea kabisa kwa kuwa amechoshwa na hatua ya kuuzwa kwa mkopo kila mwaka. (A Bola, via Goal)
Arsene Wenger anasema kwamba majuto yake makubwa akiifunza Arsenal ni kushindwa kumsaini mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi. (beIN Sports)
Mkufunzi wa taasisi ya soka ya Crystal Palace Shaun Derry amefichua jinsi siku nne za kuichezea klabu ya Cambridge United zilivyomfanya beki wa England Aaron wan Bissaka kushawishika kuanza safari yake kuelekea Man United. . (Standard)
TETESI ZA SOKA JUMANNE
Juventus imekataa kumuuza winga Douglas Costa 28 licha ya Man United kuwa na hamu ya kumsajili baada ya mkufunzi Maurizio Sarri kuzuia uhamisho wa nchezaji huyo wa Brazil. (Mail)
Real Madrid itawasilisha ombi la kumsaini kiungo wa kati wa Tottenham Christian Eriksen msimu ujao iwapo Paul Pogba ataongeza kandarasi yake na Man United .
Eriksen mwenye umri wa miaka 27 atapatikana kwa uhamisho wa bila malipo kwa kuwa kandarasi yake inakamilika 2020. (Sky Sports)
Beki wa Real Madrid Sergio Ramos amemshauri Pogba, 26, kutoka Man United na kuhamia katika klabu hiyo ya Uhispania. (Express)
Chelsea imeanzisha mazungumzo na beki wa Itali Emerson, 25, kuhusu kandarasi mpya mpya. Winga wa England Callum Hudson Odoi 18 anakaribia kukamilisha mkataba mpya wa malipo ya £180, 000 kwa wiki katika mkataba wa miaka mitano.. (Express)
Tottenham iliwatuma wawakilishi ili kumtazama mshambuliaji wa Fenerbahce Vedat Muriqi, 25, akiichezea Kosovo wikendi iliopita.
Maskauti kutoka Lazio, Fiorentina na Napoli pia walikuwepo huku Muriqi akifunga katika ushindi wa Kosovo wa 2-1 dhidi ya Czech Republic. (Sabah, via Four Four Two)
Mlinda lango wa Manchester United David de Gea, 28, anakaribia kutia kandarasi mpya ambayo itampatia mshahara wa £290,000 kwa wiki ikiwa ni mshahaha anaolipwa Pogba. (Guardian)
Mchezaji wa timu ya Itali ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 21 Paolo Nicolato amemwambia mshambuliaji wa Everton Moise Kean kujifunza kutokana na makosa baada ya kuwasili kuchelewa katika mkutano wa timu kabla ya mechi dhidi ya Ubelgiji.
Kean 19 aliwachwa nje kutoka katika kikosi cha Itali katika mechi za kimataifa za hivi karibuni (Gazzetta Dello Sport, via Sport Witness)
Tottenham ilitaka kumsaini kiungo wa kati wa Roma Nicolo Zaniolo, 20, kulingana na ajenti wa mchezaji huyo kabla ya kumsaini Giovani lo Celso kwa mkopo badala yake. (Mail)
Wolves ilifeli kumsaini kiungo wa kati Leeds Kalvin Phillips msimu huu ,ilibainika baada ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 kutia kandarasi mkataba mpya katika klabu hiyo.. (Football Insider)
Chelsea imeambia maajenti wake wakuu kwamba inaamini kwamba marufuku ya uhaimsho waliowekewa inayowazuia kununua wachezaji msimu huu itapunguzwa , ikimaanisha kwamba wanaweza kununua wachezaji katika dirisha la uhamisho la mwezi Januari.. (Mirror)
Kiungo wa kati wa Newcastle Jonjo Shelvey, 27, ametaja baadhi ya ukosoaji dhidi Steve Bruce na klabu hiyo kama upuzi na aibu. (Chronicle)
Klabu ya ligi ya Bundelsiga Paderborn huenda inataka kufanya jaribio la pili la kumsaini kiungo wa kati wa Crystal Palace Jairo Riedewald, 23, mnamo mwezi Januari baada ya kukosa uhamisho wa mkopo msimu huu . (Football.London)
Beki Jesus Vallejo, 22, aliyejiunga na Wolves kwa mkopo katika dirisha la uhamisho la msimu huu anaweza kuuzwa na klabu ya Real Madrid msimu ujao. (Birmingham Mail)
Tamasha kwa jina A Cirque du Soleil kuhusu mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi liitaanza katika mji wa Catalan mwezi Oktoba. (Standard)
TETESI ZA SOKA JUMATATU
Barcelona wanaandaa mkataba mpya wa mshambuliaji Lionel Messi, 32, ambao utambakisha nyota huyo Camp Nou kwa miaka iliyosalia ya maisha yake ya soka. (Mundo Deportivo via Mirror)
Chelsea inaweza kulazimika kumpa mkataba wa muda mrefu beki wake wa kushoto Mbrazil Emerson Palmieri, mwenye umri wa miaka 25, ambaye kocha Maurizo Sarri anamyemelea kumpeleka Juventus. (Express)
Manchester United na Manchester City wapo mbioni kupambana kumsajili kiungo wa wa Benfica Florentino Luis mwenye umri wa miaka 20. (Star)
Kiungo nyota wa Ufaransa Paul Pogba, 27, aliamua kusalia Manchester United badala ya kuhamia Real Madrid kutokana na mkataba wa pauni pauni 150 wa udhamini wa michezo . (The Sun)
Beki wa timu ya taifa ya Uholanzi Virgil van Dijk, 28, ameshangazwa na maneno kuwa atapewa ofa ya mpya ya mkataba wa malipo ya pauni na 200,000 kwa wiki na klabu yake ya Liverpool. (Liverpool Echo)
- Robert Mugabe 'Zimbambwe ni huru daima'
- Kwa nini Instagram inawagharimu zaidi maharusi?
- Harmonize afunga ndoa kwa siri bila WCB
- Je, unafahamu kuwa mihogo ni miongoni mwa vyakula vyenye sumu?
Kiungo wa Lazio Sergej Milinkovic-Savic, 24, anakaribia kusaini mkataba mpya licha ya Manchester United kumtaka Mserbia huyo pamoja na vilabu vya Paris St-Germain na Juventus. (Daily Mail)
Meneja wa zamani wa Leicester Mfaransa Claude Puel ndiye mtu anayetazamiwa kuchukua nafasi ya meneja katika klabu ya Ureno ya Sporting Lisbon.(L'Equipe)
Marcos Rojo, 29, atalazimisha kuhamia Aston Villa kutoka Manchester United mwezi Januari , baada ya mlinzi huyo wa Argentina kushindwa kuondoka Old Trafford katika dirisha la usajili lililoisha hivi karibuni. (Birmingham Live)
- Tetesi za soka Ulaya Jumapili 08.09.2019
- Tetesi za soka Ulaya Jumamosi 07.09.2019
- Barca haitamsaini Neymar
Kelechi Nwakali, 21, ambaye alihamia katika klabu ya daraja la pili ya Uhispania, Huesca kutoka Arsenal msimu huu , anataka kurudi katika uwanja wa Emirates siku zijazo . (Score Nigeria via Football.London)
Beki wa England Danny Rose, 29, anataka kuendela kupigania nafasi yake katika timu ya Tottenham Hotspur licha ya kwamba klabu nyingine zimeonyesha kumtaka na kuwasili kwa Ryan Sessegnon, mweny umri wa miaka 19, kutoka Fulham. (Mirror)
Real Madrid watagrejelea tena haja yao ya kumsaka kiungo wa kati wa Ajax - Donny van de Beek,mwenye umri wa miaka 22, katika kipindi cha msimu kuhama kwa wachezaji cha majira ya kiangazi cha mwaka 2020 . (Daily Mail)
Leeds wanakaribia kabisa kuongeza zaidi mkataba wa miaka mitano na kiungo wa kati wa Kalvin Phillps mwenye umri wa miaka 23 ,baada ya Aston Villa na Burnle kuonyesha nia za kumnunua mchezaji huyo katika kipindi cha mechi za kipindi cha kabla ya kuaza kwa msimu wa michezo . (Telegraph)
Mchezaji wa safu ya nyuma wa Italy ukipenda full-back -Matteo Darmian, mwenye umri wa miaka 29, anasema hajutii kitendo chake cha kuhamia Manchester United,paada ya kujiunga na Parma kuhfuatia misimu minne akiwa katika Old Trafford. (Football Italia)
Mlinda lango wa Stalwart Germany na Bayern Munich Manuel Neuer, mwenye umri wa miaka 33, hana mipango ya kustaafu . (Mirror)
Waziri mkuu wa Albania Edvin Rama amefichua kuwa mwenzake wa Ufaransa Emmanuel Macron aliomba msamaha wa dhati baada ya kupigwa kwa wimbo wa taifa ambao sio wa Albania kwa ajili ya timu ya nchi yake katika mchezo wa timu zilizofuzu kwa ajili ya kombe la Euro 2020 wakati wapocheza na timu ya Ufaransa mjini Paris. (Goal.com)
0 Comments