Tetesi za Soka Ulaya Jumatatu 02.09.2019:

Neymar
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionNeymar
Barcelona wamesitisha jaribio lao la kutaka kumsajili mshambuliaji wa kimataifa wa Brazil Neymarkutoka Paris Saint-Germain hadi msimu ujao. (ESPN)
Mazungumzo kati ya vilabu hivyo yalivunjika baada ya PSG kulegeza masharti yao licha ya Neymar kujitolea kulipa £17.7m kufikia makubaliano ya usajili wake. (Sky Sports)
Mshambuliaji wa Colombia Radamel Falcao alipokelewa na mashabiki 25,000 alipowasili Istanbul siku ya jumapili kabla ya pendekezo la kujiunga Galatasaray kutoka Monaco. (Mirror)
Roma wanamatumaini ya kusaini kiungo wa kati wa Arsenal Henrikh Mkhitaryan ,30. (Sky Italy - in Italian)
Henrikh MkhitaryanHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionHenrikh Mkhitaryan
Beki wa zamani wa Liverpool Martin Skrtel amevunja mkataba wake na Atalanta inayoshiriki Ligi ya Serie ya Italia wiki kadhaa baada ya kujiunga na klabu hiyo. (Mail)
Mshambuliaji wa Frankfurt mwenye umri wa miaka 25 Mcroatia Ante Rebic anajiandaa kujiunga na AC Milan, huku mshambuliaji Andre Silva, 23 Mreno akitarajiwa kujiunga na klabu hiyo. (Goal)
Kipa wa Paris St-Germain Alphonso Areola, 26, anatarajiwa kumilisha uhamisho wake kwenda Real Madrid siku ya mwisho katika mkataba ambao utamwezesha kipa wa Costa Rica Keylor Navas, 32, kujiunga na klabu hiyo. (Mirror)
Andre SilvaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
PSG wanataka kumsajili mshambuliaji wa Argentina Mauro Icardi, 26, kwa mkopo kutoka Inter Milan. (RMC Sport - in French)
Mlinzi wa Bayern Munich Mjerumani Jerome Boateng, 30, anakaribia kujiunga na mabingwa wa Italia uventus. (Bild, in German)
Juventus bado wana matumaini ya kumsaini kiungo wa kati wa Barcelona wa miaka 31 Mcroatia Ivan Rakitic - na huenda wakatoa ofa ya kumuachilia mchezaji wa kiungo cha kati Mjerumani Emre Can, 25, kama sehemu ya kufikia mkataba wa kumsajili Ivan Rakitic. (Sport - in Spanish)
Ivan RakiticHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Meneja wa Napoli Carlo Ancelotti anasema kuwa yuko tayari kumsaini mshambuliaji wa Uswidi Zlatan Ibrahimovic, 37, kutoka LA Galaxy. (Sun)
Borussia Dortmund wanapigiwa upatu kumsajili kipa wa Liverpool wa miaka 18 Bobby Duncan ikiwa klabu hiyoo ya Ligi Kuu ya Uingereza ataamua kukomesha mkataba wake . (Mirror)

Tetesi Bora Jumapili

Kiungo wa kati wa Ufaransa Paul Pogba, 27 anaweza kukataa kusaini mkataba mpya na Manchester United ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kusajiliwa Real Madrid. (Mirror)
Kiungo wa kati wa Ufaransa Paul Pogba, 27Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionKiungo wa kati wa Ufaransa Paul Pogba, 27
Ingawa meneja wa Unites Ole Gunnar Solskjaer amedai kuwa Pogba atasalia Old Trafford.(Express)
Bayern Munich inataka kumsaini winga wa Mancity Leroy Sane licha ya kwamba winga huyo mwenye umri wa miaka 23 atauguza jeraha la muda mrefu(Mirror)
Alexis Sanchez, 30,amejiunga na Inter Milan katika mkataba wa muda mrefu wa mkopo baada ya meneja wa Manchester United, Solskjae kumwambia kuwa mchezaji huyo anaweza kuchezea mashindano ya vikombe na ligi ya ulaya.(Sun)
Alexis Sanchez, 30,Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionAlexis Sanchez
Mshambuliaji wa inter Milan Mauro icardi 26 ametishia kuishtaki klabu hiyo ya ligi ya serie A kwa kuwa mchezaji kiungo wa Argentina hana raha kuondolewa katika kikosi cha Kwanza cha timu hiyo.
Mshambuliaji wa West Ham na Javier Hernandez, 31, ametuma maombi yake ya kuhamia Sevilla.(Mail)
Mpango wa Christian Eriksen kutoka Tottenham kwa paundi milioni 72 kwenda PSG imegonga mwamba baada ya Neymarameamua kubaki kwa mabingwa wa ligue 1. (Sun)
erikHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES

Post a Comment

0 Comments