China yaripoti visa vipya 4 vya maambukizi ya virusi vya corona

Nchini China kumeripotiwa visa vipya vinne vya maambukizi ya virusi vya corona kwa Aprili 29, ikiwa ni pungufu ya vingine 22 vilivyobanika siku moja kabla.

 Kwa mujibu wa mamlaka ya afya ya nchi hiyo visa vyote hivyo ni kutokoka mataifa ya nje. Idadi jumla ya maambukizi hadi wakati huu imefikia watu 82,862, pasipo na kisa kipya cha kifo.

Kwa hivyo idadi jumla ya vifo nchini humo inasalia kuwa 4,633.

Post a Comment

0 Comments