Helkopta ya NATO yapoteza mawasiliano Ugiriki

Helkopta ya Canada chapa CH-148 Cyclone ambayo ilikuwa katika mpango wa ulinzi wa Umoja wa Kujihami wa NATO imetoweka katika maeneo ya bahari kati ya Ugiriki na Italia.

 Katika taarifa yake jeshi la Canada limesema ilipoteza mawasiliano wakati ikiwa katika doria zake kawaida na kwamba jitihada za uokozi zinaendelea.

Hata hivyo taarifa hiyo haijaeleza ilikuwa na watu wangapi, ingawa awali jeshi la Uigiriki lilisema inaaminika ilikuwa na watu sita.

Taarifa za awali zinasema ilikuwa umbali wa maili 50 kutoka kisiwa cha Kefalonia cha Ugiriki.

Post a Comment

0 Comments