Jack Ma: Bilionea anayejaribu kumaliza virusi vya corona na kurejesha hadhi ya China kuwa juu

Mfanyabiashara Ma ni kichocheo cha operesheni inayoendelea ya kusambaza vifaa vya kimatibabu ambayo hadi kufikia sasa zaidi ya nchi 150 zimefaidika
Tajiri zaidi China alifungua akaunti yake ya Twitter mwezi uliopita, katikati ya mlipuko wa janga la corona. Hadi kufikia sasa, wanaomfuata wamejitolea katika kampeni ya kuwasilisha vifaa vya kitabibu dhidi ya ugonjwa wa covid 19 kwa karibu kila nchi kote duniani.
"Dunia moja, kupambana kwa pamoja!" Kujitolea ni moja ya ujumbe wa kwanza wa Jack Ma "Pamoja, tutafanikiwa!" alisema.
Mfanyabiashara huyo tajiri ndio kichocheo cha operesheni inayoendelea ya kusambaza vifaa vya kimatibabu ambayo hadi kufikia sasa zaidi ya nchi 150, zimepokea barakoa na mashine za kupumua.
Lakini wakosoaji wa Ma na hata baadhi ya wanaomuunga mkono hawajaelewa nia yake. Je tajiri huyu amejitoa kama Rafiki wa chama tawala cha China cha Kikomunisti? Au je ni mshirika binafsi anayetumiwa na chama hicho kwa nia za propaganda?
Anaonekana kufuata sheria za kidiplomasia za China, hasa wakati anapochagua ni nchi gani itafaidika na msaada wake, lakini nguvu yake inayoendelea kuongezeka huenda ikamuweka kwenye njia panda dhidi ya viongozi wenye wivu katika ngazi ya juu ya kisiasa nchini China.
Mabilionea wengine pia wameahidi kutoa msaada zaidi katika kukabiliana na janga la virusi vya corona - huku mkurugenzi na mwanzilishi mwenza wa mtandao wa Twitter Jack Dorsey akiahidi kutoa $1bn (£0.8bn). Shirika la Marekani linalofuatilia michango inayotolewa na mashirika ya kutoa misaada limemuweka Alibaba katika nafasi ya 12 katika orodha ya wachangiaji wakubwa binafsi katika kukabiliana na janga la corona.
Lakini orodha hiyo haijumuishi usambazaji wa vifaa vya msingi ambavyo baadhi ya nchi wanavichukulia kuwa na umuhimu mkubwa hata kuliko pesa katika kipindi hiki cha kukabiliana na mlipuko wa virusi vya corona.

Hakuna mwingine kati yao zaidi ya Ma ameweza kusambaza vifaa vya msingi kwa wanaohitaji moja kwa moja. Kuanzia Machi, Jack Ma mwanzilishi wa kampuni ya Alibaba alianza kusambaza bidhaa za msingi za kukabiliana na corona kwa Afrika, Asia, Ulaya, Amerika Kusini na hata kwa nchi zenye siasa nyeti kama vile Iran, Israel, Urusi na Marekani.
Ma pia amewasilisha msaada wa mamilioni ya pesa katika utafiti wa chanjo dhidi ya virusi vya corona na kijitabu kidogo cha wataalamu wa tiba kwa madaktari katika mji wake wa Zhejiang kimefasiriwa kutoka Kichina hadi nchi zingine 16. Lakini meli za usambazaji wa vifaa vya kimatibabu ndio kumekuwa mada katika vyombo vingi vya habari duniani na kumfanya Ma hata kuendelea kuwa maarufu.
"Ana uwezo na pesa na uwezo wa kupata ndege itakayoondoka mji wa Hangzhou nchini China hadi Addis Ababa, au popote kule anapotaka iende," anaelezea mwandishi wa wasifu wa Ma, Duncan Clark. "Huu ni utaratibu; hivi ndivyo ilivyo kwa kampuni, watu wake na mji wake."
Mtu Rafiki
Jack Ma anafahamika kama mwalimu wa lugha ya Kiingereza mwenye haiba kubwa ambaye alianzisha kampuni kubwa ya teknolojia. Alibaba kwasasa anafahamika kama "Amazon ya Mashariki".
Ma alianzisha kampuni ndani ya nyumba yake ndogo pwani ya China mji wa Hangzhou, katikati ya eneo la kiviwanda 1999. Tangu wakati huo, Alibaba amekuwa akiendelea kukua na kuwa miongoni mwa washikadau wakuu katika nchi hiyo ambayo ni ya pili kiuchumi duniani, akiwa amekumbatia zaidi nyanja ya kimtandao China, benki na burudani.
Thamani ya Ma ni zaidi ya dola bilioni 40.
2018, alijiondoa rasmi kama mwenyekiti wa kampuni ya Alibaba na kusema kwamba sasa ataangazia zaidi masuala ya misaada. Lakini Ma amedumisha nafasi yake kama mwanachama wa kudumu katika bodi ya kampuni hiyo. Utajiri wake na umaarufu wake umemfanya kuendelea kuwa maarufu nchini China.

Post a Comment

0 Comments