Mkuu wa Wilaya ya Mtwara amefariki Dunia “alikuwa na changamoto ya upumuaji”

Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Evod Mmanda amefariki Dunia jana saa tano usiku katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara (Ligula), Waziri wa TAMISEMI Selemani Jafo amesema Mmanda aliugua na kulazwa kwa siku mbili na alikuwa anasumbuliwa na changamoto ya upumuaji.

“DC wa Mtwara Evod Mmanda amefariki majira ya saa tano usiku jana Hospitali ya Mkoa wa Mtwara(Ligula), ameanza kuugua juzi amelazwa kwa siku mbili na shida kubwa ni kwamba alikuwa na changamoto ya upumuaji, ni pengo kubwa alikuwa Mwanasheria mzuri na mchapakazi, mwili bado upo Hospitali Ligula, RC Mtwara anaratibu mazishi”-WAZIRI JAFO

Post a Comment

0 Comments