Tetesi za soka Ulaya Alhamisi 30.04.2020: Reguilon, Pochettino, Sane, Sancho, Ndombele, Pedro, Edouard

Arsenal wameripotiwa kuwasiliana na Real Madrid kuhusu uhamisho wa beki wa Uhispania Sergio Reguilon, 23, ambaye yupo Sevilla kwa mkopo. (ABC, via Star)
Mauricio Pochettino ni chaguo la kwanza la mmiliki mtarajiwa wa Newcastle kuchukuwa nafasi ya mkufunzi Steve Bruce na wako tayari kumlipa £19m kwa mwaka. (Sky Sports)
Mkufunzi wa Bayern Munich Hansi Flick amefanya mazungumzo ya simu ya dakika 30 na winga wa Manchester City na Ujerumani Leroy Sane, 24, kujadili uwezekano wa uhamisho wake. (Bild, via Goal - in German)
Leroy Sane
Winga wa Borussia Dortmund na England Jadon Sancho, 20, amepewa ofa ya nafasi saba na Manchester United katika juhudi za kumshawishi ajiunge na klabu hiyo. (Mirror)
Kiungo wa Ufaransa Tanguy Ndombele, 23, anatathmini hatima yake ya baadae katika klabu ya Tottenham, huku Barcelona wakimmezea mate. (Sky Sports)
Mkufunzi wa Roma Paulo Fonseca anataka kumsajili winga wa Chelsea na Uhispania Pedro, 32. (Corriere dello Sport - in Italian)
Jadon SanchoHaki miliki ya pichaEPA
Arsenal wameambiwa lazima walipe zaidi ya £25m ikiwa wanataka kumnunua mshambuliaji wa Celtic na Ufaransa Odsonne Edouard, 22. (Express)
Mshambuliaji wa Napoli Dries Mertens, 32, anataka kuhamia London, huku Chelsea ikiwa bado inamnyatia kiungo huyo wa kimataifa wa Ubelgiji. (Mail)
Leicester inataka kumsajili beki wa Saint-Etienne Mfaransa Wesley Fofana, 19. (Le10 Sport - in French)
Wesley Fofana wa Saint EttieneHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
AC Milan huenda ikamuuza kipa wa zamani wa Uhispania Pepe Reina, dirisha la uhamisho litakapofunguliwa. Kipa huyo wa miaka 37- sasa yupo kwa mkopo Aston Villa. (Calciomercato)
Nigel Pearson atasalia kama mkufunzi wa Watford, hadi mwisho wa msimu licha ya kuwa mkataba wake unamalizika mwezi Mei. (Sky Sports)
Arsenal ina mpango wa kufanya uhamisho wa bure na mkataba wa kubadilishana wachezaji dirisha la uhamisho litakapofunguliwa msimu wa joto kutokana na changamoto za kifedha zilizochangiwa na janga la corona. (Mail)
Kiungo wa kati wa Chelsea Itali Jorginho, 28, amedokezea uwezekano wake kuondoka klabu hiyo baada ya kuchezea Blues kwa msimu mmoja kutokana na ukosoaji unaomkabili kutoka kwa mashabiki. (FourFourTwo)

Post a Comment

0 Comments