Tetesi za soka Ulaya Jumatano 29.04.2020: Pogba, Aubameyang, Ozil, Rice, Van de Beek, Rodriguez

Manchester United huenda wakalazimika kumuuza kiungo wa kati wa Ufaransa Paul Pogba, 27, kwa bei ya chini kutokana na athari za janga la corona katika mchezo wa soka. (Goal)
Arsenal watamuuza mshambuliaji wa Gabon Pierre-Emerick Aubameyang, 30, kwa dau la £30m kwasababu hawataki aondoke klabu hiyo kwa uhamisho wa bila malipo. (Sun)
Gunners bado haijampatia mkataba mpya kiungo wa kati wa Ujerumani Mesut Ozil, 31. (ESPN)
Mesut Ozil
West Ham inatarajiwa kukataa ofa iliyowasilishwa na Chelsea ya kumnunua kiungo wa kati wa England Declan Rice, 21. (Goal)
Newcastle na Everton wanang'ang'ania saini ya kiungo wa kati wa Ajax na Netherlands Donny van de Beek. Manchester United na Real Madrid pia wamehusishwa na nyota huyo wa miaka 23. (Le10 Sport - in French)
Everton wamempatia ofa ya mkataba wa miaka minne kiungo wa kati wa Real Madrid na Colombia James Rodriguez, 28. (Mundo Deportivo - in Spanish)
James RodriguezHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Arsenal na Manchester United wanataka kumsajili mshambuliaji wa Monaco na Ufaransa Wissam Ben Yedder, 29. (L'Equipe - in French)
Everton imefanya mazungumzo na Barcelona kumhusu beki wa miaka 20 Jean-Clair Todibo. Kinda huyo wa Ufaransa sasa yupo Schalke kwa mkopo. (Mail)
Liverpool imeanza mazungumzo na wawakilishi wa mshambuliaji wa Lille na Nigeria Victor Osimhen, 21. (Le10 Sport - in French)
Victor Osimhen
Image captionLiverpool imeanza mazungumzo na wawakilishi wamshambuliaji wa Lille na Nigeria Victor Osimhen
Newcastle wanapania kumbadilisha mkufunzi wao Steve Bruce with Flamengo na Jorge Jesus, ambaye aliongoza klabu hiyo ya Brazil mwaka 2019 kushinda taji la Copa Libertadores. (Goal)
Arsenal italazimika kuilipa Real Madrid euro milioni 50 sawa na (£44m) wakitaka kumsaini kwa mkataba wa kudumu kiungo wa kati wa Uhispania Dani Ceballos, 23, ambaye anachezea klabu hiyo kwa mkopo. (AS - in Spanish)
Arsenal wanajizatiti kumzuia winga wao wa miaka 18, Bukayo Saka anayenyatiwa na klabu zingine za Ligi ya Primia asiondoke, kwa kumpatia mkataba mpya. (90min)
Bukayo Saka
Chelsea wanataka kumsaini kiungo wa kati wa Paris St-Germain Mfaransa Kays Ruiz-Atil,17, ambaye mkataba wake unamalizika 2021. (L'Equipe - in French)

TETESI ZA SOKA JUMANNE

Pogba na Lingaard
Manchester United wako tayari kumuuza kiungo wa kati wa Ufaransa Paul Pogba, 27, na kiungo wa kati wa England Jesse Lingard, 27, kumnunua Sancho. (Sun)
Mkurugenzi wa michezo wa Borussia Dortmund anasema "amenyamaza " kuhusu hatma ya baadae ya Jadon Sancho. Winga huyo wa England, 20, amehusishwa na tetesi za kuhamia Manchester United. (Sport1 - in German)
Mshambuliaji wa Everton Moise Kean, 20, amehusishwa na tetesi za kuhamia Napoli.
Mtaliano huyo huenda akachukuliwa hatua za kinidhamu na Everton kwa kukiuka muongozo wa serikali wa kukabiliana na coronavirus mapema wiki hii. (Corriere dello Sport - in Italian)
Moise KeanHaki miliki ya pichaAFP
Wachezaji nyota wa Barcelona Philippe Coutinho, 27, na Ousmane Dembele, 22, wako tayari kujumuishwa kwa mkataba wa kubadilishana wachezaji msimu huu. (Telegraph - subscription required)
Chelsea walimtaka Coutinho lakini sasa wanamnyatia kiungo matata wa Bayer Leverkusen na Ujerumani Kai Havertz, 20. (Athletic - subscription required)
Arsenal wamewasilisha ofa ya £43m kumnunua kiungo wa kati wa Atletico Madrid na Ghana Thomas Partey, 26. (Express)
Thomas ParteyHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Liverpool wanapigiwa upatu kumsajili mshambuliaji wa Lille Victor Osimhen, 21, ijapo kuwa Leicester na Chelsea pia wanamng'ang'ania raia huyo wa Nigeria . (Le Foot Mercato - in French)
Arsenal wamekosa nafasi ya kumsajili kiungo wa kati wa Manchester United wa miaka 15 Omari Forson kwa mkataba wa kitaalamu. (Mail)
Manchester United wamehusishwa na uhamisho wa beki wa Real Valladolid na Ghana Mohammed Salisu, 21. (AS - in Spanish)
Mohammed SalisuHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Kiungo wa kati wa Leicester Wilfred Ndidi amesema anafurahia sana uwepo wake katika klabu hiyo, licha ya tetesi zinazomhusisha Mnigeria huyo wa miaka, 23, na uhamisho wa Manchester United ama Arsenal. (Teamtalk)
Kiungo wa kati wa Uhispania Dani Ceballos, 23, amesema ana matumaini ya kurejea Real Madrid mkataba wake wa Mkopo wa msimu mzima Arsenal utakapomalizika. (Movistar - in Spanish)
Mshambuliaji wa Atletico Madrid Diego Costa amesema mkufunzi wake wa zamani wa Chelsea Antonio Conte huenda "asidumu" msimu mzima katika klabu kama Real Madrid. Conte amekuwa mkufunzi wa Inter Milan tangu Mei 2019. (ESPN)
Diego CostaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Mkufunzi wa zamani wa Tottenham na Chelsea Andre Villas-Boas amesema hatarudi tena katika Ligi ya Premier. (Mail)
Mshambuliaji wa Tottenham Son Heung-min huenda akakosa mazoezi ya Ligi ya Primia. Raia huyo wa Korea Kusini, 27, ambaye yuko nyumbani kwa huduma ya kitaifa atalazimika kujitenga atakaporudi. (Evening Standard)

Post a Comment

0 Comments