Trump ataka shule za umma kufunguliwa



Rais Trump alitoa kauli hiyo katika mkutano wa njia ya simu kwa magavana waliokuwa wakijadili jinsi ya kuruhusu tena shughuli za kiuchumi kuendelea miongoni mwa masuala mengine.
Amesema "Tunapendekeza wafungue shule haraka iwezekanavyo lakini kwa tahadhari na kuzingatia usalama. Tunataka kila mtu awe salama, nadhani mutaliona hilo. Magavana wengi wanafikiria kuhusu mifumo ya shule zao, si mbali shule zitafunguliwa tena hata kama ni kwa muda mchache. Nafikiria huenda likawa jambo zuri."
Hata hivyo kwa mujibu wa shirika la habari la Associated Press, hakuna gavana yoyote aliyeridhia pendekezo hilo la kufungua shule. Maafisa wengi wa elimu wana wasiwasi kuwa huenda kukawa na hasara kubwa hata kuliko faida iwapo shule zitafunguliwa.
Shule kote nchini Marekani zimefungwa kutokana na janga la virusi vya Corona.

Post a Comment

0 Comments