Abiria 200 wasafiri kutoka Tanzania kwenda India


Hatimaye abiria 200 wakiwemo raia wa India jana usiku wamefanikiwa kusafiri kwa ndege ya Shirika la ndege la Tanzania ATCL kutoka hapa nchini kuelekea India kutokana na juhudi za ushirikiano baina ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya India kupitia Balozi zote mbili ili raia hao waweze kuungana tena na familia zao.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa ATCL Lebris Laanyuni amesema kuwa huu ni muendelezo wa jitihada za Serikali kuamua kuwarejesha nyumbani abiria walioshindwa kusafiri kutokana na zuio lililosababishwa na janga la Covid-19 na kwamba hapo awali walifanikiwa kuwarudisha nchini Tanzania abiria 246 waliokwama nchini India.

Post a Comment

0 Comments