Hatukwenda Madagascar kuchukua kikombe cha Babu ile ni dawa ya kisayansi- Waziri Kabudi

“Kile sio kikombe cha Babu, hatukwenda Madagascar kuchukua kikombe cha Babu ile ni dawa ya kisayansi, ndio maana tumeenda na Wataalamu, mimi peke yangu kwakuwa ni Waziri nimepata bahati ya kugonga ile dawa hata wenzangu hawakugonga, ila zile chupa tumekuja nazo 2 tu za kusaidia utafiti na nyingine (sio chupa) zipo kwenye Box, kwa sasa hatuna dawa za kugawa ni za utafiti”- Waziri Kabudi

“Watu waendelee kuchukua tahadhari hata kama tunaona hizi juhudi za uwepo wa matumaini ya dawa, lakini tuchukue tahadhari, hata sisi kwenye Ndege ya Rais tulikaa mbalimbali na tumevaa mask” -Waziri Kabudi

Post a Comment

0 Comments