Kufuatia mbio ambazo ni za kiuchokozi katika majaribio ya makombora na silaha za nyuklia mwaka 2017,Kim alitumia michezo ya Olimpiki ya majira ya baridi Korea kusini kuanzisha majadiliano na Marekani na Seoul mwaka 2018.
Hatua hiyo ilisababisha wimbi la mikutano, ikiwa ni pamoja na mitatu kati ya Kim na Trump.
Lakini majadiliano hayo yameshindwa katika miezi iliyopita kutokana na kutokubaliana katika kubadilishana na unafuu wa vikwazo pamoja na hatua za kuachana na utengenezaji wa silaha, ambao ulizusha shaka juu ya iwapo Kim kama ataondoa kabisa hazina yake ya silaha ambayo anaiona kuwa ni nguzo yake imara ya kuendelea na shughuli zake.
Kim aliingia katika mwaka 2020 akiapa kujenga hazina yake ya silaha za nyuklia na kuvishinda vikwazo kwa kutumia "uchumi wa kujitegemea."
Baadhi ya wataalamu wanasema hatua ya Korea ya kaskazini ya kuwazuwia watu kutoka nje katika wakati wa mzozo wa virusi vya corona kunaweza kuzuwia kwa kiasi kikubwa uwezo wake wa kuwahimiza watu kufanyakazi.
0 Comments