Kim Jong Un ajitokeza baada ya minong'ono kuhusu afya yake

Kufuatia mbio ambazo ni za kiuchokozi katika majaribio ya makombora na silaha za nyuklia mwaka 2017,Kim alitumia michezo ya Olimpiki ya majira ya baridi Korea kusini kuanzisha majadiliano na Marekani na Seoul mwaka 2018.
Hatua  hiyo  ilisababisha  wimbi  la  mikutano, ikiwa  ni  pamoja  na mitatu  kati ya  Kim na  Trump.
Lakini  majadiliano  hayo  yameshindwa  katika  miezi  iliyopita kutokana  na  kutokubaliana katika  kubadilishana  na  unafuu  wa vikwazo  pamoja  na  hatua za  kuachana  na  utengenezaji  wa silaha, ambao  ulizusha  shaka  juu  ya  iwapo  Kim kama ataondoa kabisa  hazina  yake  ya  silaha ambayo  anaiona  kuwa  ni nguzo yake  imara  ya  kuendelea  na  shughuli  zake.

Kim Jong Un katika mkutano wa wa chama tawala mjini Pyongyang Aprili 11, 2020

Kim aliingia  katika  mwaka  2020  akiapa  kujenga  hazina yake  ya silaha  za  nyuklia na  kuvishinda  vikwazo  kwa  kutumia "uchumi  wa kujitegemea."
Baadhi  ya  wataalamu  wanasema hatua ya  Korea ya kaskazini  ya kuwazuwia  watu  kutoka  nje  katika  wakati wa  mzozo wa  virusi vya  corona kunaweza  kuzuwia  kwa  kiasi  kikubwa  uwezo wake wa  kuwahimiza  watu  kufanyakazi.

Post a Comment

0 Comments