MAGUFULI: ''nitatuma ndege ikalete dawa ya corona''

Nimewasiliana na watu wa Madagascar kuna dawa kule ya corona wanasema wameipata nitatuma ndege hio dawa ije hapa tuitumie, wengine wanasema nipo Chato, hapa si ndio nilipozaliwa na hata nikifa nitazikwa hapa kuna ubaya gani nikiwa Chato? tuache siasa za ajabu

Wengine wanasema tufunge biashara au shughuli za kiuchumi wakati wengine wanaendesha magari ya STK  nainawekwa mafuta na serikali amesahau alichiokalia ndicho kinachotoa mafuta , mishahara tutalipaje tukifunga.

Wengine wako DSM wanasema watu wasiende Bungeni , na nimeagiza wasilipwe posho maana utalipwa kwa kazi uliyoifanya , kuna mambo ya ajabu yanafanyika , sina imani na Mkuu wa Maabara ya Taifa maana haiwezekani tupeleke sampuli za mapapai zioneshe zina corona''.- JPM

Post a Comment

0 Comments