Serikali ya Afrika Kusini imesema kuanzia Jumatatu itawaruhusu watu kununua pombe na kuhudhuria makanisani ikiwa ni sehemu yake ya kulegeza masharti ya kukabiliana na janga la corona. Lakini hatua hizo zitakwenda sambamba na kanuni za kujikinga katika taifa hilo lenye visa vingi vya maambukizi barani Afrika.
Na pombe hizo zitanywiwa nyumbani tu. Makanisa yatafunguliwa lakini kusiwe na mkusanyiko wa watu wanaozidi 50. Vitakasa mikono, barakoa na kujitenga baina ya mtu na mtu ni mambo ya lazima kanisani. Afrika ya Kusini ina maambukizi 25, 937 huku vifo vikiwa 552.
0 Comments