Mchezaji wa Atalanta afariki dunia

Kiungo wa Atalanta ya Italia Andrea Rinaldi aliyekuwa akicheza kwa mkopo Legnano ya Serie D, afariki dunia akiwa na umri wa miaka 19 kwa kupata tatizo katika Ubongo (aneurysm) toka Ijumaa.

Andrea Rinaldi enzi za uhai wake ameichezea Legnano aliyokuwa kwa mkopo jumla ya mechi 23 wakati katika club ya Atalanta alikuwa toka akiwa na umri wa miaka 13 na kucheza game 35 za U-17.

Rinaldi ambaye alikuwa amejiunga na Legnano toka August 2019, amefariki akiwa hospitali.

ADVERTISEMENT

Post a Comment

0 Comments