Msako wanaouza sukari bei juu kuanza leo Dar

Mkuu wa Mkoa wa DSM Paul Makonda ametangaza Operesheni ya kuwabaini na kuwakamata wafanyabiashara wanaouza Sukari kwa bei ya Juu kinyume na maelekezo ya bei elekezi ya Serikali na kuwaagiza wakuu wa Wilaya katika jiji la DSM kuanza operesheni hiyo Kesho.

Akizungumza jijini DSM, Bw. Makonda amesema pamoja licha ya wafanyabiashara kutangaziwa bei elekezi na Serikali, wamekuwa wakiendelea kuuza Sukari kwa bei ya kati ya Tsh. 3,200 hadi 4,000 kwa kilo moja huku wengine wakidaiwa kuendelea kuficha bidhaa hiyo hali ambayo inaleta usumbufu kwa wananchi.

Post a Comment

0 Comments