Msanii mpya wa Konde Gang Ibraah aachia rasmi EP

Msanii mpya chini ya Lebo ya Konde Music World Wide, @ibraah_tz ameachia rasmi Ijumaa hii Extended Play (EP) yenye ngoma tano iitwayo "Hatua" Steps.

EP hiyo iliyosheheni ngoma tano za moto, imefanyiwa mabadiliko katika moja ya ngoma ambayo ni ngoma namba 4 iitwayo 'Njiwa' na kuingizwa ngoma nyingine iitwayo 'Wandoto' kama mbadala wake.

Aidha, hadi sasa "Steps" EP iliyotoka chini ya @kondegang inaendelea kufanya vizuri kupitia platform mbalimbali hususani Boomplay.

Post a Comment

0 Comments