Natarajia kuoa hivi karibuni nishaanza mipango- Ommy Dimpoz

Mkali wa Bongofleva Ommy Dimpoz amesema yupo kwenye maandalizi, na panapo maajaliwa ataweza kufunga ndoa hivi Karibuni

Akiongea 'LIVE' na MVP Lil Ommy kupitia Ukurasa wake wa Instagram, Dimpoz amesema kua kwasasa ameanza maandalizi madogo madogo ikiwemo kufuga ndevu , ili ata akienda kuposa aonekane Ni Kijana anaejielewa
.
Mkali uyo anaetamba na Ngoma 'KATA' ameongeza kua alitaka kuoa kipindi hiki Cha Ramadhan, lakini akaogopa asije kuuziwa mbuzi kwenye gunia.

Post a Comment

0 Comments