Antonio Guterres aunga mkono kupelekwa misaada nchini Syria

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anaunga mkono kuurefusha muda wa mpango wa kupeleka misaada nchini Syria kupitia kwenye mipaka na nchi jirani.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema katika ripoti yake kwamba kupeleka misaada nchini Syria kutokea nchi jirani kutahitaji kupitia vivuko vya Bab al-Salaam na Bab al-Haw kwenye mpaka baina ya Syria na Uturuki kwa muda wa miezi 12 ijayo.
Ujerumani na Ubelgiji ziliwasilisha ombi hilo kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. Guterres ameeleza kuwa zoezi hilo litahakikisha upatikanaji wa mahitaji muhimu kwa mamilioni ya raia ambao Umoja wa Mataifa utaweza kuwafikia. Hata hivyo Urusi na China zimesema mpango huo utahujumu uhuru wa Syria. Urusi ilishauri wazo la kupeleka misaada hiyo ya kibinadamu kwa kupitia mji mkuu wa Syria Damascus.

Post a Comment

0 Comments