Kiongozi wa upinzani nchini Malawi Lazarus Chakwera ameshinda uchaguzi wa wiki hii wa rais ulioamriwa kufanyika tena kwa asilimia 58.57 ya kura, tume ya uchaguzi ya nchi hiyo imesema.
Ilikuwa ni mabadiliko makubwa ya majaaliwa kwa kiongozi aliyeko madarakani, Peter Mutharika, ambaye ushindi wake katika uchaguzi wa mwezi Mei 2019 ulibatilishwa na mahakama ya katiba, yakihusishwa na udanganyifu mkubwa.
Kiasi ya wapiga kura milioni 6.8 katika taifa hilo dogo la kusini mwa Afrika walijitokeza katika vituo vya kupigia kura siku ya Junanne. Na jana Jumamosi , tume ya mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Chifundo Kachale aliwaambia waandishi habari; "Tume imemtangaza Lazarus Chakwera , kwa kupata asilimia 58.57 ya kura, kuwa amechaguliwa kuwa rais wa Malawi.
Mutharika alikuwa wa pili kwa kupata kura 1,751,377, wakati mgombea ambaye hajulikani sana Peter Dominico Kuwani amepata kuwa 32,456.
0 Comments