Trump anavyoikosoa VOA, ushahidi tosha ni chombo huru cha habari

Rais Donald Trump akihojiwa na Mwandishi wa VOA Greta Van Susteren June, 12, 2018, Singapore.

Kwa Sauti ya Amerika (VOA) mtendaji mkuu wa habari ambaye alifanya maamuzi mazito, habari ya kipekee na ilikuwa si ya kawaida kuiacha ipite tu.
Siku 10 tu baada ya mashambulizi ya Septemba 11 nchini Marekani ambayo yaliua Wamarekani 2,977 na kujeruhi wengine kadhaa, mshirika wa karibu sana wa Osama bin Laden na mlinzi wake nchini Afghanistan, kiongozi Mullah Omar -- alifanya mahojiano maalum na Idhaa ya Pashto ya VOA.
Myrna Whitworth, kaimu mkurugenzi wa Sauti ya Amerika wakati huo, aliwatuma waandishi wawili wa habari kufanya mahojiano kwa njia ya simu na kiongozi wa Taliban ambaye alimruhusu bin Laden, mpangaji mkuu wa mashambulizi ya 9/11, kuwa na makazi nchini Afghanistan.
Lakini maafisa wa utawala wa Bush “waliheshimu haki ya shirika hili kuripoti bila ya upendeleo,” maafisa hawakutaka VOA ifanye “mambo ambayo tulidhani yatakuwa ni faraja kwa adui,” Richard Boucher, msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wakati huo, alisema katika mahojiano ya karibuni.
Rais George W. Bush akiongea katika sherehe za miaka 60th ya Sauti ya Amerika (VOA) Februari, 25, 2002, Ofisi za VOA Washington, DC.
Rais George W. Bush akiongea katika sherehe za miaka 60th ya Sauti ya Amerika (VOA) Februari, 25, 2002, Ofisi za VOA Washington, DC.
VOA, ambayo inafadhiliwa na serikali kuu, ni shirika la kimataifa la utangazaji, linatoa huduma kupitia zaidi ya lugha 40 kwa watu karibu milioni 280 kwa wiki. Lina historia ambayo inaanzia tangu vita vya pili vya dunia na ina mamlaka kutoka katika bunge kuripoti habari kwa kina bila ya kuelemea upande wowote.
Lakini mivutano kati ya White House na VOA imekuwa ni jambo la kawaida kwa miongo kadhaa, kiasi kikubwa kwa sababu ya hali isiyo ya kawaida ya kuwa na uhuru kiasi - na mara nyingine kutumia nguvu zaidi - shirika hili la habari linafanya kazi ndani ya himaya kubwa ya urasimu wa serikali kuu.
Rais Barack Obama akihojiwa na mwandishi wa VOA Andre DeNesnera White House
Rais Barack Obama akihojiwa na mwandishi wa VOA Andre DeNesnera White House
Mwezi uliopita, Rais Donald Trump aliungana na baadhi ya viongozi waliomtangulia ambao walielezea kutopendezwa na ripoti za VOA -- lakini kwa nguvu isiyo ya kawaida na uchangamfu.
“Kama ungesikia kile ambacho kinatoka Sauti ya Amerika, kinachukiza. Mambo, ambayo wanasema yanachukiza kwa nchi yetu,” Trump amesema wakati akiongea na wana habari kuhusu virusi vya corona kwenye eneo la Rose Garden mnamo April 15.
Malalamiko ya Trump kimsingi yalihusu masuala mawili: Kwanza, kwamba VOA ilitumia takwimu zisizo za kweli za China kuhusu maambukizi ya virusi vya corona na vifo nchini China katika ripoti zake -- shutuma ambazo zimepingwa vikali na taasisi ya habari.
Pili, rais alikuwa amekasirishwa kwamba ameshindwa kuhakikisha mkuu mpya aliyemteua kuongoza taasisi kuu ya VOA - U. S Agency for Global Media - kwa kipindi cha zaidi ya miaka miwili kwasababu ya vikwazo vya wademokrat kumthibitisha katika baraza la Senate.
Trump awali alilalamika juu ya ukosefu wa udhibiti wa chombo cha habari ambacho kinamilikiwa na serikali na kinaashiria thamani yake na ile ya wafuasi wake. Novemba mwaka 2019, Trump alipendekeza kwamba Marekani ni vyema iwe na chombo kinachoendeshwa, kinachosambaza habari ulimwenguni ili kukabiliana na kile alichokiita habari ambazo ‘si haki” na “za uongo” kutoka CNN na kuionyesha dunia jinsi nchi hii ilivyo ‘nzuri.”
Hata hivyo, kama mahojiano ya Mullah Omar na mifano mingine inavyoonyesha, Trump si rais wa kwanza kukosoa ripoti za VOA. Hiyo ni kwa sababu wakati taasisi ya habari kwa kawaida inaongozwa na mtu anayeteuliwa na White House, habari zinazofanywa na waandishi waliobobea katika taaluma hiyo wanatakiwa kisheria kutoelemea upande wowote.
Mabadiliko ya Uhariri katika Shirika la Utangazaji la Serikali
White House na Wizara ya Mambo ya Nje wamekataa ombi la VOA kuelezea zaidi juu ya ukosoaji wa rais uliotangazwa katika televisheni au katika shutuma tofauti ambazo zimeelezewa kwa kina katika kijarida cha White House mapema mwezi huu, ambapo iliishutumu VOA kwa kukuza propaganda za wachina katika matumizi yake ya takwimu wakati wa janga la virusi vya corona.
Mkurugenzi wa VOA Amanda Bennett alilipinga dai hilo na kusema shirika “linajitahidi kuripoti bila ya kupigia debe habari ya upande wowote.”
Kwa hakika, VOA ilielezea udhaifu wa China kwa habari zisizo za kweli karibu mara 20, kwa mujibu wa Kamati ya Wanahabari, kundi ambalo linatetea uhuru wa habari.
Rais John Kennedy alipotembelea Sauti ya Amerika Mwaka 1962.
Rais John Kennedy alipotembelea Sauti ya Amerika Mwaka 1962.
Mwelekeo huu wa uhariri siku zote haukuwa ni sera ya VOA. Baada ya shirika hili kuundwa mwaka 1942 kupambana na propaganda za Nazi kwa habari maalum, katika miongo ya kwanza ya VOA kuripoti ambapo ilikuwa ni kwa idhini ya wahusika katika serikali.
Wakati wa enzi ya Kennedy mzozo wa kombora la Cuba mwaka 1962, VOA kimsingi ilikuwa ikifanya kazi “chini ya uangalizi wa serikali,” amesema Nicholas Cull, profesa wa diplomasia ya umma katika chuo kikuu cha Southern California Annenberg katika chuo cha elimu ya Mawasiliano na Uandishi wa Habari na mwandishi wa kitabu “The Cold War na Idara ya Habari ya Marekani.”
“Kulikuwa na afisa utawala aliyepelekwa VOA kutoka idara ya habari ya Marekani,” amesema Cull. “Alikuwa anaidhinisha kila habari.”
Mwelekeo huo ulivurugika wakati wa kashfa ya Watergate ambayo ilipelekea Rais Richard Nixon kujiuzulu mwaka 1974. Cull amesema kwamba waandishi wa habari wa VOA ambao walisisitiza kutoa picha kamili kuhusu uchunguzi kuhusiana na shutuma kuwa rais alifanya makosa walipata upinzani kutoka kwa maafisa wa USIA ambao walitaka habari chanya zaidi.
Waandishi walitaka suala la Watergate liwe ni “somo la uraia litangazwe kuonyesha kwamba nguvu ya Marekani haiko kwa rais kwamba hajawahi kufanya kosa, lakini uwezo wa Bunge kusahihisha kosa hilo kupitia mchakato unaostahili,” amesema Cull. Mwishowe, muafaka ulifikiwa kwamba kila wakati kama kuna habari mbaya kuhusu rais, habari nzuri ni vyema itolewe pia.
“Hii ilipelekea aina fulani ya matangazo ya ajabu,” amesema Cull. “Walikuwa wakisema, katika habari hivi leo Rais ametajwa kuwa ni mhusika ambaye hatashtakiwa katika mgogoro wa Watergate… na Mke wake Bi Nixon amefungua shule mpya ya watoto hapa Washington DC.”
Shirika la Habari lilizuiliwa kuonyesha upendeleo
Mnamo mwaka 1976, Bunge na watendaji wa VOA waliazimia kuwa shirika hilo linahitaji mamlaka ya wazi ya uhariri kuhakikisha kwamba wanadumisha uaminifu wao kwa wasikilizaji wa nje. Bunge liliandika rasimu ya Muongozo, ambayo inasema VOA lazima itangaze habari za uhakika; iwe na habari ambazo zinawakilisha jamii ya wamarekani wote; na kutoa maelezo ya wazi na majadiliano kuhusu sera za Marekani.

Post a Comment

0 Comments