Umoja wa Afrika wakemea matumizi ya nguvu Marekani


Musa Faki Muhammed , kiongozi wa Umoja wa Afrika ametolea wito Marekani  kuondoa kila jambo ambalo linaviashiria  vya ubaguzi.

Umoja wa Afrika kupitia kiongozi wake Musa Faki Muhammed umetoa wito kwa Marekani kuingilia kati na kuondoa viashiro vyote ambavyo vinaonekana kuwa ni vitendo vya kibaguzi nchini Marekani.

Katika taarifa yake ya maandish, Muhammed Musa Faki amekemea  ghasia  na ukiukwaji wa haki wa maafisa wa jeshi la Polisi Minneapolis na kitendo kilichopelekea kuuawa kwa mmarekani mweusi .

Musa Faki ametoa salamu za rambi rambi kwa  familia ya George Floyd, mmarekani aliuawa kwa kukandamizwa na goti shingoni na askari ambae bila shaka hakuwa na roho ya kibinadamu.

Kiongozi huyo wa Umoja wa Afrika amekumbusha kuwa wakati wa kuanzishwa Umoja wa huo,  ulikuwa ukikemea  matendo ya kibaguzi tangu mwaka  1964 .

Musa Faki ameendelea akisema kwamba  viongozi nchini Marekani wanatakiwa  kuongeza juhudi zao katika jitihada za kuzingatia  usawa na kuebuka  aina yeyote ya ubaguzi wa rangi.

Umoja wa Afrika umekemea vikali  matendo ya kibaguzi dhidi ya mtu mweusi nchini Marekani.

Post a Comment

0 Comments