Jumuiya ya Kimataifa yaichangia Sudan dola bilioni 1.8

Mataifa ya magharibi na yale ya kiarabu yameahidi mchango wa dola bilioni 1.8 kuisaidia Sudan inayoandamwa na hali mbaya uchumi, tangu vuguvugu la demokrasia lilipoung´oa utawala wa muda mrefu wa rais Omar al-Bashir.
Ahadi hiyo kutoka zaidi ya mataifa 40 ikiwemo msaada wa nyongeza wa dola milioni 400 kutoka benki ya dunia, imetolewa wakati wa mkutano uliotishwa na Ujerumani kwa lengo la kuisaidia serikali ya mpito nchini Sudan baada ya miongo kadhaa ya vikwazo vya kiuchumi na kutengwa kimataifa chini ya utawala wa al-Bashir.
Waziri wa Mambo ya kigeni wa Ujerumani Heiko Maas aliuambia mkutano huo uliofanyika kwa njia ya video kuwa msaada uliotolewa ni hatua ya kwanza ya kuisaidia Sudan na kwamba kutakuwa na mkutano mwingine wa wafadhili mapema mwaka unaokuja.
Akitoa ahadi ya mchango wa Ujerumani kwa Sudan waziri wa ushirikiano wa kiuchumi na maendeleo wa serikali ya shrikisho Gerd Muller amesema:
"Tayari kwa sehemu tumechukua hatua kwenye maeneo ya kipaumble ya ajira na mafunzo ya ufundi, usalama wa chakula na utowaji wa huduma za msingi. Tutaendelea kutanua ushirkiano huu zaidi, pamoja na mwenzangu Heiko Maas ninaahidi kwa niaba ya serikali ya Ujerumani msaada jumla wa euro milioni 150 kwa Sudan kwa mwaka 2020"

Post a Comment

0 Comments