Hong Kong:Waandamanaji watawanya kwa gesi ya kutoa machozi



Watetezi wa demokrasia katika jiji hilo wameukosoa vikali mswada huo wa sheria ambao pia unapinga kujiingiza kati kutoka nje katika mambo ya ndani ya jimbo hilo lenye mamlaka ya utawala wa ndani. Wapinzani wa sharia hiyo wanasema inaenda kinyume cha kanuni ya nchi moja mifumo miwili, inayohakikisha uhuru wa jimbo la Hong Kong usiokuwapo China bara.
Makundi ya waandamanaji waliovaa nguo nyeusi walikusanyika ili kuupinga mswada huo wa sheria. Watu hao walitoa kauli mbiu za kusisitiza msimamo wa pamoja na ukombozi wa Hong Kong. Watu wapatao 120 walikamatwa na polisi kwa kujiunga na mikusanyiko isiyoruhusiwa.
Polisi wamesema waandamanaji waliwarushia mawe na kuwapulizia unyevunyevu usiojulikana. Kwa mujibu wa taarifa ya polisi maafisa wanne walijeruhiwa. Hapo awali, mwanaharakati maarufu Tam Tak-Chi alikamatwa kwa madai ya kushiriki katika mikusanyiko isiyoruhusiwa.
Hata hivyo mwanaharati huyo amesema alikuwa anatoa nasaha juu ya masuala ya afya na kwamba alikuwa na ruhusa ya kufanya hivyo. Mswada wa sheria uliosababisha maandamano ya leo uliwasilishwa kwenye bunge la China ijumaa iliyopita na unatarajiwa kupitishwa tarehe 28 ya mwezi huu.

Post a Comment

0 Comments