Ndugai yuko sahihi kuwakatalia CHADEMA- Msekwa

Spika Mstaafu Pius Msekwa amesema, uamuzi wa Spika Ndugai wa kukataa kuvuliwa Ubunge kwa Wabunge 4 wa CHADEMA ni sahihi kwa kuwa Bunge ni muhimili unaojitegemea kimaamuzi.

Msekwa amesema kupishana kwa uamuzi kati ya CHADEMA na Bunge hakuna tatizo, sawa sawa na chama cha siasa kupishana maamuzi na muhimili wa Mahakama.

"Kwa uzoefu wangu wote wawili CHADEMA na Bunge wote wako sahihi kwenye maamuzi yao, inavyoonekana maamuzi yanapingana lakini kila upande una mamlaka yake, kupingana si jambo la ajabu hata Mahakama huwa zinapingana" amesema Spika Mstaafu.

"Spika ameeleza kwanini anaona shida kukubali uamuzi huo na anasababu zake, sababu unaweza kwenda mahakamani na Mahakama ikakataa uamuzi wako, kwa sababu ya njia tu ulizozitumuia" ameongeza Spika Mstaafu Msekwa.


ADVERTISEMENT

Post a Comment

0 Comments