Ujerumani kuruhusu tena mikusanyiko ya ibada

Wajerumani wataruhusiwa tena kukutana kwa ibada, kupeleka watoto wao kwenye bustani za mapumziko pamoja na kutembelea majengo ya makumbusho. Marufuku ya hafla za mikusanyiko mikubwa ya watu itaendelea kuwepo.
Kansela wa Ujerumani Angela Merkel pamoja na wakuu wa majimbo 16 nchini humo wamekubaliana kupunguza zaidi vikwazo vilivyokuwa vimewekwa kuzuia kuenea kwa maambukizi ya virusi vya corona.
Kulingana na Kansela Merkel, viwanja vya michezo vya watoto, majengo ya makumbusho, pamoja a bustani za maua na wanyama zitafunguliwa tena lakini kwa masharti maalumu. Ameongeza kwamba hatua nyingine zitatangazwa ifikapo Mei 6. Aidha Merkel ameonya kwamba Ujerumani lazima ijitahidi kushusha zaidi idadi ya maambukizi mapya ya kila siku na kwamba sheria ya kuweka umbali kutoka mtu mmoja hadi mwingine lazima izingatiwe katika maeneo ya umma ili kuzuia kuongezeka kwa maambukizo.
Aidha maeneo ya ibada kama vile makanisa na miskiti pia itafunguliwa tena. Hafla zingine za kidini, ikiwa ni pamoja na harusi, kubatizwa na mazishi pia zinaruhusiwa. Majimbo yote ya nchini Ujerumani yatalazimika kuhakikisha tahadhari za kujikinga na maambukizi hayo zinatekelezwa. Mikusanyiko ya kidini tayari imesharuhusiwa katika majimbo ya Saxony na Thuringia nchini humo.

Mikahawa haitofunguliwa

Merkel amesema kufungua mikahawa wakati huu itakuwa shida kwa sababu, ni vigumu kujua iwapo watu waliokaa meza moja ni kutoka familia moja, au kutoka familia tofauti.

Post a Comment

0 Comments