Vikwazo vyaanza kulegezwa Ulaya, New York

Virusi vya corona vimewauwa zaidi ya watu 283,000 kote duniani tangu mripuko kutokea China mwezi Disemba. Zaidi ya visa milioni nne vya maambukizi vimeripotiwa katika nchi 195 duniani.

Kati ya hao zaidi ya milioni nne walioambukizwa, zaidi ya watu milioni moja na laki tatu wamepona virusi hivyo.

Baadhi ya sehemu za Ulaya na hata mji wa New York huko Marekaniimeanza kulegeza vikwazo taratibu ila ongezeko la maambukizi China na Korea Kusini ni jambo linalomkumbusha kila mmoja kuhusu hatari ya wimbi la pili la maambukizi. Shirika la afya la Duniani WHO limeonya kuhusiana na hatari ya kulegeza vikwazo kwa haraka. Tedros Adhanom Ghebreyesus ni mkurugenzi wa WHO.

"Kuondoa vikwazo ni muhimu kwa kuinua chumi kwa ajili ya kulinda maisha, ila pia ni muhimu kuviangalia kwa jicho la karibu virusi hivi ili hatua za kuvidhibiti ziweze kuchukuliwa endapo kutakuwa na ongezeko la visa," alisema Tedros.

Idadi ya wanaofariki Uhispania imepungua mno

Lakini huku mamilioni ya watu wakiwa wamepoteza ajira zao kutokana na virusi hivyo vya corona na uchumi wa nchi mbalimbali ukiwa umeathirika vibaya, serikali zinataka sana kuharakisha mambo yarudi sawa sawa.


ADVERTISEMENT


Post a Comment

0 Comments